Anusurika kuchinjwa katika ugomvi wa wakulima Wilaya ya Kiteto

Kiteto:Bahati ni kweli ana
bahati kama jina lake lilivyo Bahati. Katika mapigano, yaliyotokea hivi
Karibuni, mtoto, Bahati Juma alikuwa ni mmoja wa watu waliojikuta wako
katikati ya mapigano hayo.
Mtoto huyu anasema alikamatwa na kundi la wafugaji
wa Kimasai, akiwa ndani ya nyumba yao iliyochomwa moto. Katika tukio
hilo, Bahati alinusurika kufa ingawa tayari sime ilikuwa imeanza kukata
shingo yake.
Hivi sasa Bahati amelazwa katika Hospitali ya
Wilaya ya Kiteto, Mkoa wa Manyara, akiuguza jeraha la kukatwa na sime na
ameshonwa nyuzi nane huku akiwa na majeraha ya fimbo mgongoni na
mikononi.
Ndugu zake watatu ambao ni wakulima wote kutoka
mkoani Dodoma, wameuawa ambao ni Juma Mlangwa (47) na Yohana Hivo (33)
waliuawa papohapo na Mussa Juma alifariki akiwa hospitali.
Katika mapigano hayo yaliyotokea Desemba 21 Kijiji
cha Olpopong, wakulima wengine wanane walijeruhiwa, mmoja alikuwa
mahututi. Mussa Juma ambaye alichomwa mkuki wa mbavu, alihamishiwa
hospitali ya Mkoa ya Dodoma, alifariki baadaye.
Wengine waliolazwa hospitali ya wilaya ya Kiteto
ni Emanuel Mathias (26), Hoti Damas (38), Mwajuma Hamis (20), Habiba
Ally(16 ) na Mwajuma Martin(33).
Daktari azungumza
Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya wilaya ya Kiteto, Thomas Ndalio anasema, hali za majeruhi hao saba zinaendelea vizuri.
“Mussa ndio hali yake ilikuwa mbaya sana na ndio
sababu alihamishiwa Hospitali ya Mkoa wa Dodoma kwa matibabu zaidi, kwa
bahati mbaya alifariki,”anasema Dk Ndalio.
Bahati asimulia alivyonusurika kifo
Anasema, anakumbuka Desemba 21 alikuwa nyumbani na ndugu zake, wakiwa wamepumzika baada ya kutoka shamba kulima.
Siku hiyo anakumbuka kulikuwa kumezuka mgogoro
katika eneo la malisho kati ya wakulima na wafugaji wa jamii ya Kimasai.
Wafugaji hao walikuwa wameingiza katika mashamba yao, mifugo na
walifanikiwa kuwafukuza.
(CHANZO MWANANCHI)
(CHANZO MWANANCHI)
No comments:
Post a Comment